Serikali ya
Tanzania imesema mauzo ya kahawa katika msimu wa mwaka 2018/2019 yamewezesha
kuliingizia Taifa dola za Marekani milioni 123 sawa na takriban Sh283.7
bilioni.
Naibu Waziri
wa Kilimo, Bw.Omary Mgumba aliyekuwa
akizungumza (Novemba 12, 2019) Bungeni amesema hadi kufikia mwisho wa msimu wa
2018/2019 kiasi cha tani 66,646 cha kahawa kiliuzwa ikiwa ni asilimia 102.8 ya
makisio ya uzalishaji wa tani 65,000.
“Kati ya tani hizo zilizouzwa, tani 41,971 zimeuzwa kupitia
minada ya kahawa na 24,575 zimeuzwa katika soko la moja kwa moja,”
amesema Bw.Mgumba.
Mauzo hayo
yaliwezesha kuliingizia Taifa takriban Sh283.7 bilioni yakiwa yameshuka
ikilinganishwa na msimu wa 2017/2018 ambapo mauzo yalikuwa Sh341 bilioni
Huenda
mapato yatokanayo na uuzaji wa kahawa yakaendelea kupungua hata katika msimu wa
mwaka 2019/2020, baada ya Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB) kusema uzalishaji wa
zao hilo utashuka kutokana na mzunguko mdogo na kuchelewa kwa mvua katika mikoa
ya kanda ya kaskazini ikiwemo Kilimanjaro na Arusha.
Katika
taarifa ya Hali ya Sekta ya Kahawa Tanzania iliyotolewa na TCB mwezi April 2019
inaeleza kuwa matarajio ya uzalishaji wa kahawa katika msimu ujao wa 2019/2020
yatakuwa tani 50,000 ambapo ni sawa na upungufu wa asilimia 23.6 ukilinganishai
na uzalishaji wa mwaka 2018/2019.
Aidha,
Serikali imewahakikishia wakulima wa kahawa nchini kuwa mifumo ya mauzo ya moja
kwa moja pamoja minada katika mikoa ya Kilimanjaro na Songwe, Ruvuma, Njombe, Kagera inayotumika
msimu wa 2019/2020 itaendelea kutumika nchini.
|
0 Comments