Na Wiliam Mpanju – RK Biharamulo.
Baadhi ya
wakazi na Wafanyabiashara wa soko la zamani Kasusula
maarufu soko la Wakuilma mjini Biharamulo, wilaya
ya Biharamulo mkoani
Kagera wamelalamia hatua ya idara ya Mazingira wilayani humo, kuanza kuchoma taka kwenye
dampo la jirani na soko hilo badala ya kuziondoa na
kuzipeleka eneo la kuhifadhia taka nje ya mji huo hali iliyosababisha
moshi wa taka hizo kuwa kero kwa wananchi.
Mara
kadhaa taka hizo zimekuwa zikipigiwa kelele na Wananchi
kwa kusababisha harufu mbaya kutokana na madampo hayo kuwa
karibu na maeneo ya makazi, mighahawa na maeneo wanakouzia bidhaa za
vyakula lakini bado halmashauri imeshindwa
kutekeleza hata agizo alilolitoa mkuu wa wilaya hiyo Bi
Sada Malunde baada ya Wananchi kulalamika.
Kufuatia
kushindwa kuzolewa kwa taka hizo maafisa
mazingira wanatuhumiwa kuchoma taka hizo ambazo
moshi wake unadaiwa kuwa chanzo cha uchafuzi wa mazingira na
kudaiwa kuwa kero kwa wafanyabiashara wa soko
hilo na mamalishe ambapo Radio kwizera
imeshuhudia moshi mkubwa ukifuka eneo hilo na kusambaa maeneo
mbalimbali ya mjini huo na afisa mazingira alipotafutwa hakuweza
kupatikana na simu yake iliita bila kupokelewa.
|
0 Comments