![]() |
Shirika la
World Vision Tanzania limekabidhi majengo yaliyojengwa na mradi wa World
Vision(Izigo AP) kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji Kabuleme, Kata Izigo,
Wilaya ya Muleba,mkoani Kagera.
|

![]() |
Akipokea
majengo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba, Ndg. EMMANUEL SHEREMBI ameendelea kushukuru sana shirika la
World Vision Tanzania kwa kuendelea kufadhili miradi mbalimbali iliyotekelezwa
na inayoendelea kutekelezwa wilayani Muleba ikiwemo ujenzi na ukarabati wa
zahanati ya Bushekya, ujenzi wa zahanati Bugasha, ujenzi wa miundombinu shule
ya msingi Kabuleme na ujenzi wa jengo la mama na mtoto kituo cha afya Izigo.
"Msichoke
kutufadhili katika sekta za Elimu na Afya kwani Wilaya ya Muleba ina uhaba
mkubwa sana wa miundombinu ya Elimu na Afya hali inayopelekea jamii kukosa
huduma hizo za muhimu. Serikali imekuwa ikijitahidi kuboresha miundombinu hiyo
lakini bado uhitaji ni mkubwa", ameeleza Ndg. EMMANUEL SHEREMBI.
|

![]() |
Majengo
yaliyokabidhiwa ni pamoja na vyumba vitatu vya madarasa vyenye thamani ya Tzs.
60,132,210.00 ambapo Shirika la World Vision limechangia Tzs. 54,512,210.00 na
jamii imechangia Tzs. 5,620,000.00, ujenzi wa matundu matano ya vyoo na ununuzi
wa tanki la maji wenye thamani ya Tzs. 14,693,360.00, ununuzi wa madawati 60
kwa jumla ya Tzs. 5,160,000.00 na ununuzi wa mipira 6 ya michezo yenye thamani
ya Tzs. 435,000.00. Jumla ya gharama za ujenzi na vifaa ni Tzs.80,420,560.00.
Imetolewa
na:
Kitengo cha Habari, Mawasiliano na Mahusiano,
Halmashauri
ya Wilaya ya Muleba.
|

0 Comments