![]() |
Na Luteni Selemani Semunyu, JWTZ
Gavana wa benki kuu ya Tanzania Profesa
Florens Luoga anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi katika mashindano ya wazi ya golf Tanapa
Lugalo open yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Juni 22 katika Viwanja vya
Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania wa Lugalo Jijijini Dar es Salaam.
Hayo yabainishwa na Mwenyekti wa Klabu ya Jeshi
la Ulinzi la wananchi wa Tanzania la Lugalo Brigedia Jenerali Mstaafu Michael
Luwongo kupita taarifa nakwamba Gavana huyo Profesa Florens Luoga amethibitisha
kushiriki kufunga mashindano hayo.
Amesema kukubali kwa Gavana Profesa Luoga
kuwa mgeni rasmi katika mashindano hayo ni faraja kwa Klabu ya Gofu ya
lugalo ambayo ndio imepewa dhamana ya kuandaa mashindano hayo ambayo yanasomeka
katika kalenda ya TGU.
Kwa upande wake mtunza Viwanja Greeen keeper
David Helela alisema kazi ya kuweka Alama katika viwanja (Mark() imekamilika na
kichachosubliwa sasa ni upangaji wa droo na kutangazwa ili kila mmoja aweze
kutambua kuwa yuko katika Nafasi gani na muda gani wa Mchezo
|
![]() |
“Uwanja
uko katika hali Nzuri na Wachezaji wanaendelea na mazoezi ya mwisho ili
kuhakikisha mashindano yanakuwa mazuri kwa Upande wao na kuibuka na Ushindi
mnono”.
Baadhi ya wachezaji wa Vilabu mbalimbali
wameonekana katika Viwanja vya Lugalo wakifanya mazoezi ya mwisho kujiandaa na
michuano hiyo ambayo kwa ijumaa itaanza kwa Wachezaji wa kulipwa na Wachezaji
wasaidizi huku Jumamosi na jumapili ikisalia kwa wachezaji wa ridhaa.
Mashindano hayo yatashirikisha
wachezaji wa Ridhaa na wa Kulipwa katika makundi yote ikiwemo Wanawake Wazee na
Watoto sambamba na Wachezaji wasaidiizi ambao watapata nafasi katika Siku ya
kwanza ya Mashindano.
Mashindano hayo yanayodhaminiwa na Mamlaka
ya Hifadhi za taifa TANAPA ili kuunga mkono Jitihada za Serikali kukuza michezo
na gofu ina muunganiko na Utalii hivyo wanaimani kupitia Gofu pia itakuza
uchumi kutokana na kukua kwa Utalii.
Mashindano ya Lugalo open hufanyika
kila mwaka kwa mujibu wa kalenda ya TGU na Klabu ya JWTZ ya Lugalo
imekuwa ikipewa dhamana ya Kuyaaandaa.
|
0 Comments