Source; RK: BF [Takwimu Malaria]
ED: AG
Date: Friday, October 18,
2019
NGARA
Maambukizi ya ugonjwa wa
malaria wilayani Ngara Mkoani Kagera yamepanda kwa mwezi Septemba mwaka huu,2019 kwa
asilimia 50.1 ukilinganisha na mwezi Agosti ambapo yalikuwa ni asilimia 49.1.
Akizungumza na redio kwizera
Mratibu wa Malaria wilaya ya Ngara, Dkt.Madina Kibiriti amesema kiwango cha
ugonjwa kimeonekana kupanda kila mara kutokana na wananchi kushindwa kutumia
vyandarua na kufuata sheria za usafi.
Dkt. Madina amesema matumizi
ya vyandarua kwa wananchi ni asilimia 85 kwa takwimu za Mwaka jana 2018,
zilizopatikana wakati wa unyunyiziaji wa dawa ya ukoko majumbani kuanzia mwazi
Oktoba hadi Disemba.
Kwa upande wao baadhi ya
Wananchi wilayani Ngara wamesema wamekuwa wakijikinga na ugonjwa huo hasa kwa
kufanya usafi wa Mazingira ikiwemo kufukia madimbwi katika sehemu zao za Makazi
na kutumia vyandarua jambo ambalo limekuwa likipelekea kuishi salama.
Source; RK: Faraja,M (Upepo)
ED: AG
Date: Friday, October 18,
2019
KAHAMA
Mkuu wa wilaya ya Kahama
mkoani Shinyanga ameliagiza Jeshi la Polisi wilayani humo kumkamata na kumhoji
Diwani wa Kata ya Kashishi halmashauri ya Msalala Bw. Samweli Magema kwa tuhuma
za kumuoa binti mwenye miaka 19 aliyekuwa akisoma kiato cha pili katika shule ya
Sekondari Bulige.
Mkuu wa wilaya ya Kahama Bw.
Anamringi Macha amesema taarifa za Diwani huyo kuishi kinyumba na Mwanafunzi
huyo kwa zaidi ya wiki mbili, zimetolewa October 17,2019 na Wananchi wa kijiji cha
Mwambuko.
Bw. Macha amesema baada ya
kupata taarifa hizo waliamua kwenda nyumbani kwa Diwani Magema majira ya saa
moja usiku ambapo walimkuta binti huyo na kumchukua hadi kituo cha Polisi kwa
uchunguzi zaidi huku wakiacha taarifa za kumtaka Diwani huyo ajisalimishe
Polisi.
Kwa upande wake Afisa
Mtendaji wa Kata ya Kashishi Bi. Sophia Yusuphu amesema baada ya kuzipata
taarifa hizo waliamua kutoa taarifa ngazi ya wilaya kwa hatua zaidi na kwamba
kumekuwepo na matukio mengi ya wanafunzi wa kike kukatisha masomo na kwenda
kuolewa.
ED: AG
Date: Friday, October 18,
2019
GEITA
Wanafunzi 39 wa shule ya
Ihumilo kata ya Nkome Mkoani Geita wamenusurika kifo baada ya kujeruhiwa na
radi wakati wakiwa darasani.
Kwa mujibu wa Mganga Mkuu wa
mkoa wa Geita Dkt. Japhet Simeo amesema wanafunzi watatu kati yao wanaendelea
na matibabu katika hospitali ya wilaya ya Geita iliyopo kata ya Nzera,
Wanafunzi 21 wameruhisiwa kurudi nyumbani baada ya afya zao kuimarika huku
wengine 15 waliofikishwa katika zahanati ya Nkome wametibiwa na kuruhusiwa.
Hata hivyo, Mganga mfawidhi
wa hospitali ya wilaya ya Geita Bw.
Kaitila Mrusuli amesema majeruhi hao watatu waliolazwa katika hospitali
hiyo wanaendelea vizuri na kwamba muda wowote wataruhusiwa kurudi nyumbani.
Mkuu wa mkoa wa Geita
Mhandisi Robart Gabriel amesema serikali inaendelea kuangali njia nzuri ya
namna ya kuweka tahadhari ya radi katika majengo yote ya serikali ili kuepusha
ajali za radi.
Source; RK: Sam M. (mimba mashuleni)
ED: AG
Date: Friday, October 18,
2019
KAKONKO
Serikali wilayani Kakonko
Mkoani Kigoma kwa kushirikiana na Mashirika yasiyo ya kiserikali yajipanga
kukomesha tatizo la mimba mashuleni kwa kuwapatia wananfunzi elimu ya afya ya
uzazi
Akiongea na Redio Kwizera
kupitia Bonanza la Michezo kwa kuwakutanisha Wanafunzi kutoka shule mbali mbali
za Sekondari, Mratibu wa Afya ya Uzazi Shule za Sekondari wilayani humo Bw.
Majaliwa Tryphone amesema lengo kuu ni kuhakikisha vijana hao wanakuwa na
uelewa wa namna ya kujikinga na mihemko ya mwili wakiwa bado wako shuleni
Aidha amesema baada ya kuanza
kwa mabonanza hayo kwa kushirikiana na Shirika la World Vision, tatizo la mimba
shuleni limepungua hivyo ni jukumu lao kuendelea kukabiliana na tatizo hilo.
Nao baadhi ya Wanafunzi
wilayani Kakonko wamesema elimu ambayo wamekuwa wakipatiwa imewasaidia kutambua
haki zao na kutokubali baadhi ya vitendo vya unyanyasaji ikiwemo ukeketaji kwa
watoto wa kike kutoka kwenye baadhi ya maeneo hapa nchini.
Source; RK: wm (matokeo)
ED: AG
Date: Friday, October 18,
2019
BIHARAMULO
Halmashauri ya wilaya ya
Biharamulo mkoani Kagera kupitia idara ya elimu msingi imesema imepokea matokeo
ya mtihani wa darasa la saba kwa furaha kubwa baada ya kushika nafasi ya tisa
kitaifa na nafasi ya pili kimkoa ikitanguliwa na manispaa ya Bukoba.
Afisa Elimu Taaluma wilaya ya Biharamulo Bw. Amos Nyamutela amesema hayo wakati akiongea na
Radio Kwizera baada ya kutangazwa kwa
matokeo ya mtihani darasa la saba kitaifa na wilaya ya Biharamulo ikawa ndani
ya shule kumi bora kitaifa zilizofanya vizuri katika matokeo
hayo.
Amesema ushindi huo wa awamu
ya saba mfululizo umetokana na jitihada za Walimu, Wanafunzi na Wazazi katika
kushirikiana mambo mbalimbali ikiwemo ufundishaji, na jitihada za wazazi katika
kutimiza wajibu wao kwa kuwapatia vifaa vya shule
Nao baadhi ya Walimu Wakuu wa Shule za msingi Wilaya ya Biharamulo, wamesema ushindi huo umeiletea heshima
wilaya ya Biharamulo na shule za msingi na kwamba jitihada hizo zitaendelea ili
kuhakikisha wilaya inashika nafasi ya kwanza kitaifa katika miaka ijayo.
|
0 Comments