![]() |
Waziri wa
Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako anabainisha hayo wakati wa
makabidhiano ya Miradi ya ukarabati wa shule hizo 17 yaliyofanyika katika shule
ya sekondari ya Wavulana Sengerema, wilayani Sengerema Mkoani Mwanza ambapo
amesema ukarabati huo umefanywa kwa kutumia fedha za Serikali.
Prof. Ndalichako amesema ukarabati wa shule hizo 17
zilizosimamiwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania ni utekelezaji wa mpango kabambe wa
serikali wa kukarabati shule zote 89 kongwe za serikali ambapo amesema mpaka
sasa tayari shule kongwe 46 zimeshakamilika.
Amesema Serikali inaendelea na
utekelezaj awamu ya tatu ya mpango huu ambapo shule nyingine 17 zitakarabatiwa
mwaka huu wa fedha.
|
![]() |
Akizungumzia
ukarabati wa huo Waziri Ndalichako amesema kama uamuzi wa uboreshaji wa
mazingira ya kufundishia na kujifunzia katika shule kongwe usingefanyika mapema
kungeweza kutokea majanga kwani hali ya miundombinu ilikuwa katika hali mbaya
kwenye hasa katika mifumo ya umeme, maji safi na taka na mapaa mengi yalikuwa
yameoza kabisa.
Prof. Ndalichako amesema serikali inaendelea
kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji ambapo alitolea mfano katika
mwaka wa fedha ulioisha wa 2018/19 serikali kupitia Mradi wa Lipa kulingana na
Matokeo EP4R ilitenga na kutoa fedha ambazo ziliwezesha kujengwa kwa madarasa
1,208, mabweni 222, matundu ya vyuo 2,141 na nyumba za walimu 99 pamoja na
kutatua changamoto ya huduma ya maji safi ambapo katika baadhi ya shule visima
vilichimbwa.
Shule 17
zilizokarabatiwa kwa uratibu wa TEA ni pamoja na Shule ya sekondari ya Dodoma,
Mwenge Sekondari Singida, Sekondari ya Wasichana Ruvu, Kilakala Sekondari na
Shule ya Sekondari Ilboru.
|
0 Comments