
![]() |
" Nipende kutumia FURSA HII kuwakumbusha Tena
mwezi wa Ramadhani ni mwezi mwema unapoisha tunatakiwa kuishi kwa kumcha Mungu ili tufanikiwe. Hivyo basi tunapojinda na sikukuu ya Eid el Fitr tunapaswa
kusherehe kwa Amani".
|

![]() |
Katika
iftar hiyo waislam walimuomba , Mkuu wa Wilaya mambo makuu matatu kwa
maendele ya wilaya. Mambo hayo ni changamoto kubwa zinazokikabili jamii ya
Wilaya ya Buhigwe kwa ujumla.
i.
Kuomba kuwa na eneo maalumu lililotengwa kwa ajili ya kuzikia.
ii.
Kuomba kuwepo kwa eneo maalum kwa ajili ya machinjio Wilayani
iii.
Kuomba ukubwa wa eneo wa hekari 10 kwa ajili ya kujenga chuo cha ufundi
kitachotoa elimu ya ufundi kwa jamii yote ya wana buhigwe.
|
![]() |
Iftar ili
kamalika kwa Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe kuongea na waislamu pamoja na wageni
waalikwa,kwa kuwasilisha ahadi ya fedha taslimu
shilingi laki moja kati ya shilingi laki mbili za waislamu wa Buhigwe
zilizoahidiwa kwenye Harambee ya ununuzi wa vyombo vya usafiri kwa ajili ya Jeshi
la Polisi wilayani humo ili kuunga juhudi na jitihada ya Mkuu wa Wilaya
Katika kuliwezesha Jeshi la Polisi Katika kufanya kazi vizuri, Pia Sheikh wa
Wilaya ya Buhigwe aliwaongoza wageni waalikwa kwenye kuliombea Taifa letu Amani
Pamoja na kumpongeza MKUU WA WILAYA kwa jambo alilolifanya, Kwani
halikuwahi kufanyika hapo awali.
|
0 Comments