Januari
hadi Oktoba mwaka huu,2018 mkoa wa Kagera waliojitokeza kupima afya zao
walikuwa watu milioni 1.3 kati yao watu
16,048 walikutwa na maambukizi sawa na asilimia 1.2.
Kutoa
elimu kuhusu namna ya kuepuka ugonjwa huo, mkoa wa Kagera umefanikiwa kupunguza
maambukizi kutoka asilimia 1.6 kwa mwaka 2017.
Taarifa
ya mkoa wa Kagera imeeleza kuwa Wilaya ya Misenyi ina Maambukizi ya asilimia 1.8, Ngara asilimia 0.5, Muleba asilimia1.7 , Biharamulo
asilimia1.0 Bukoba Vijijini asilimia 1.7
Bukoba Manispaa asilimia1.7 ,hivyo Jamii kutakiwa kuwa na
uaminifu katika ndoa zao.
Katika
kampeni ya Furahisha ya mkoani Kagera iliyofanyika September,2018,
watu waliojitokeza kupima walikuwa 741
kati yao wanawake walikuwa 349, wanaume 392 waliokutwa na maambukizi ya Virusi
vya UKIMWI ni wanaume watatu na wanawake watano.
Aidha,Shirika
la afya duniani WHO linasema, watu Milioni 37 duniani, wanaishi na maambukizi
ya ukimwi huku vijana wakiendelea kuwa hatarini zaidi kuambukizwa hasa barani
Afrika.
Pia Watu
wengine Milioni 22 walioambukizwa, wanatumia dawa ya AVRs ambayo imesaidia watu
wengi sana kuendelea kuishi.
|
0 Comments