Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini Tanzania
Dr Anna Peter Makakala akiwa wilayani Ngara,mkoani Kagera –Picha na Maktaba
yetu.
Maafisa Watano
wa Idara ya Uhamiaji Wilayani Ngara Mkoani Kagera wamefikishwa Mahakama ya
wilaya hiyo kwa tuhuma za kufanya shambulio kwa wakazi wa kata ya Kabanga
wakitekeleza majukumu ya kuwasaka Wahamiaji haramu.
Mbele ya
hakimu wa mahakama ya Wilaya ya Ngara Andrew
Kabuka mwendesha mashtaka wa Jeshi la Polisi Jumanne Maatu amesema Maafisa hao wametenda kosa hilo May 2,2018
katika mji wa Kabanga na kufanya vitendo vya udhalilishaji kisha kupora Mali za
raia ambayo thamani yake haijajulikana.
Bw. Maatu amewataja watuhumiwa hao kuwa ni John Johannes mwenye miaka 29, Joseph Richard mwenye miaka
32, Hussein Mungunji mwenye miaka 30, Johakimu Joseph miaka 33 na Said Ally mwenye umri wa miaka 38 na kwamba wote
wanatuhumiwa kutenda kosa la jinai kwa kuvunja
kifungu cha sheria namba 241 sura ya 16 ya mwaka 2002.
Hata hivyo
watuhumiwa wote kwa pamoja wamekana shtaka linalowakabili kwa kesi namba 115 na
116 ya mwaka 2018 na wako nje kwa dhamana ambapo hakimu wa mahakama ya wilaya Andrew Kabuka ameahirisha kesi yao hadi
May 18,2018 itakaposikilizwa tena.
|
0 Comments