![]() |
Mwenyekiti
wa kijiji cha Mukalinzi Richard Magogoro alisema hali ya ulinzi na usalama
inaridhisha baada ya kuletwa askari polisi kufanya kazi ya kutokomeza uhalifu
kwa kushirikiana na wananchi kuimarisha amani na utulivu.
Amesema
ujenzi wa kituo cha polisi unategemea
kugharimu Sh15 milioni pia kila mwananchi anachangia Sh10 000 baada ya
watu wengi kuathiriwa na matukio ya
ujambazi uliosababisha watu 17 kupoteza
maisha kati ya mwaka 2009 hadi 2016.
“Matukio ya
uhalifu yamesababisha watu kupoteza
maisha na wengine kuhama maeneo haya na baadhi walijeruhiwa na majambazi lakini
tuliopo tumechangia Sh6 milioni na kituo hadi sasa kimegharimu Sh 9 Milioni”
Amesema Magogoro.
Aidha amesema
wananchi wanaiomba serikali
kuwajengea mnara wa mawasiliano kwani majambazi hutumia changamoto hiyo kuvamia
kijiji kisha kuhatarisha usalama wakijua
hakuna taarifa zinazoweza kupelekwa
jeshi la polisi kwa haraka kupitia njia ya simu za mkononi.
Naye Mkuu wa
polisi wa wilaya ya Ngara, Abeid Maige aliwahimiza wananchi kushirikiana na
jeshi la polisi kwa kufanya doria za mara kwa mara na kutii sheria bila shuruti
huku wakitoa taarifa dhidi ya watu wanaohofia kuhatarisha usalama.
Amesema
kituo hicho kitahudumia vijiji vitatu vya kata ya Muganza lakini pia vijiji
jirani vya Murubanga, Nyamagoma na Magamba vilivyopo kata ya Murusagamba na
kwamba wajihadhari na kukaa na raia wa kigeni kutoka nchi jirani ya Burundi.
Kijiji cha
Mukalinzi kata ya Muganza wilayani Ngara chenye wakazi 10,228 waishio katika
kaya 1060 kinapakana na nchi jirani ya Burundi ambapo kimekuwa kikabiliwa na
matukio ya ujambazi kwa baadhi ya watu kuuawa kwa risasi na wengine kujeruhiwa
au kuhama makazi yao.
|
0 Comments