Rais Dkt.
John Pombe Magufuli ameamuapisha Mhe. Doto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri wa
Madini, Ikulu Jijini Dar es Salaam leo Jumatatu, Januari 8, 2018, asubuhi.
Baada ya
kuapishwa, Mhe. Dotto Biteko amesema;-“Kwanza
namshukuru Mungu kwa siku ya leo na
namshukuru kwa kuweza kutokea haya yote.
Nakushukuru wewe Mheshimiwa rais kwa
kuweza kuniteua, sina la kukupa ila kutenda kazi kwa bidii.
Mhe. Rais nina
bahati kubwa sana na hata wewe umelishuhudia kwenye mikutano mingi sana,
umenipa sifa kubwa kwa kuhudumu chini ya mwanamke ambaye ni mchapa kazi sana.
Niko tayari kufanya kazi kwa bidii na namuomba Mungu usije jutia uamuzi wako,”
alisema
Biteko.Naye
Mhe. Spika Ndugai alipota fursa ya kuzungumza akasema;-“Sisi Bunge tumekuwa
tukishauri kwa muda sana kwa serikali kuwa wizara ya nishati na madini imekuwa
wizara kubwa na nzito sana na nashukuru umeifanyia kazi kwa kuweka wizara mbili
za madini na nishati.
Tunakushukuru sana mheshimiwa Rais. Mhe. Dotto ni
mchapakazi na ana utumishi uliotukuka,” alisema Ndugai.
|
0 Comments