
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC), Jaji Mkuu mstaafu wa Zanzibar, Hamid Mahmod Hamid.
Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC), imesema kuwa uchaguzi mdogo katika majimbo ya Siha
mkoani Kilimanjaro na Kinondoni mkoani Dar es Salaam pamoja na Kata nne za
Tanzania Bara utafanyika Februari 17, 2018 kufutia waliokuwa Wabunge katika
majimbo hayo kujivua uanachama na kukosa sifa za kuendelea kuwa Wabunge.
Kwa mujibu
wa taarifa ya Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mkuu
mstaafu wa Zanzibar, Hamid Mahmod Hamid imeeleza kuwa pamoja na majimbo
hayo, pia kata nne za Isamilo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyamagana mkoani
Mwanza, Manzase, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Madanga
Halmashauri ya Wilaya ya Pangani mkoani Tanga na Kimagai Halmashauri ya Wilaya
ya Mpwapwa mkoani Dodoma zitafanya uchaguzi mdogo .
Jaji mkuu
huyo mstaafu wa Zanzibar, Hamid Mahmoud Hamid amesema kuwa, tume hiyo
itaendesha uchaguzi huo baada ya kupokea barua kutoka kwa Spika wa Bunge la
Jamhuri ya Muungano, Job Ndugai kuhusu Jimbo la Kinondoni jijini Dar es
Salaam na Jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro kuwa wazi.
Jaji Mahmoud
amesema kuwa, barua hiyo ilieleza kuwa majimbo hayo yapo wazi baada Maulid
Mtulia aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni kujivua uanachama wa CUF na Dkt.
Godwin Mollel wa Jimbo la Siha kujiuzulu uanachama wa CHADEMA na hivyo wote
kukosa sifa za kuwa wabunge.
Pia,
ameeleza kuwa Tume ilipokea taarifa kutoka kwa waziri mwenye dhamana ya
Serikali za Mitaa ikiitaarifu Tume uwepo wa nafasi wazi za Udiwani katika kata
nne za Tanzania Bara.
0 Comments