Rais Mstaafu
wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa Chama cha
Mapinduzi(CCM) kwa miaka miwili kimefanikiwa vizuri huku akisema kuwa mwaka
2020 lazima warudi kwa wananchi na kama hawajayatimiza yale waliyowaahidi
watakwenda kuwaambia nini wananchi.
Dkt. Kikwete
Rais amesema hayo leo katika Mkutano Mkuu wa 9 wa CCM unaoendelea mjini Dodoma
ambapo pamoja na hayo ili kuwa ili uweze kufanikiwa inahitaji ujasiri kama
msemo wa Kiswahili unaosema una mkata jongoo kwa meno maana kukata jongoo kwa
meno kuna hitaji ujasiri.
“Katika
miaka miwili hii kwanza mipango walioipanga wamekwisha ifanya, ilani kwanza na
mipango waliyoibuni wenyewe ndani ya serikali ni mizuri sana, kuhusu ilani
niseme tu tumepata watu, viongozi ambao ni wasimamizi wazuri sana wa ilani ya
Chama cha Mapinduzi watekelezaji hodari ni watu makini, watu wabunifu na ni watu
jasiri maana mengine anayoyafanya yanahitaji ujasiri na ule msemo wa Kiswahili
unaosema unakata jongoo kwa meno, kukata jongoo kwa meno kuna hitaji ujasiri
lakini ndio sifa ya kufanikiwa ndani ya miaka miwili hii tumefanikiwa vizuri na
mipango tuliyokuwa nayo inaleta matumaini, inaleta matumaini kwa taifa, imeleta
matumaini kwa taifa na Chama cha Mapinduzi,” amesema Dkt. Kikwete.
“Hatimae
mwaka 2020 lazima turudi kwa wananchi tutakwenda kuwaambia nini yote yale
ambayo tuliyaahidi kuyafanya yale ya ziada ambaypo viongozi hawa walikaa ndani
ya serikali kutafakari hali ilivyo na ilani ile tulitengeneza sisi kwa uthabiti
watakapo ingia wao watakaa chini wataitazama ilani wanatengeneza mipango yao na
namna ya kutengeneza mikakati ya kutengeneza ile ilani.”
|
0 Comments