Katika mbio za kilomita 42, nafasi ya kwanza hadi ya tatu zimeshikwa na
wanariadha kutoka Kenya ambapo Duncan Kwemboi ameibuka kidedea kwa
kutumia saa mbili dakika 19 na sekunde 10 kwa wanaume huku Gladys Otero
akiongoza mbio hizo kwa wanawake akitumia saa 2 dakika 49 na sekunde 32.
Katika mbio za kilomita 21, Joel Kipmatai ameshinda kwa upande wa wanaume
akitumia saa moja dakika 6 na sekunde 19 huku upande wa wanawake Merci Kibarus
pia kutoka Kenya akiibuka kidedea kwa kutumia saa 1 dakika 15 na sekunde 40
huku nafasi ya tatu ikishikwa na mtazania Failuna Abdi ambaye amezidiwa
sekunde 13 na mshindi wa kwanza.
Washindi katika mbio hizo wamejinyakulia zawadi za fedha taslimu shilingi
milioni tano kwa mshindi wa kilomita 42 na milioni 3 kwa mshindi wa kilomita
21.
|
0 Comments