
Salamu za pongezi za Rais Magufuli amezitoa kupitia ukurasa wake wa Twitter-Dr John Magufuli
kwa kuandika, “Nalipongeza
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa kutimiza miaka 53
tangu kuanzishwa kwake. Kwa kipindi chote hiki Jeshi letu limeendelea
kutimiza wajibu wake akiwa ni pamoja na kulinda amani ya nchi yetu kwa
uzalendo, umahiri, ushupavu, uadilifu na nidhamu ya hali ya juu na hivyo
kujijengea heshima ndani na nje ya nchi yetu. Najivunia kuwa Amiri
Jeshi Mkuu wa JWTZ. Mungu ibariki Tanzania, Mungu libariki Jeshi letu.”
0 Comments